Skip to main content
x
Taarifa kwa umma: yahusu mradi wa kukuza usalama wa umiliki wa ardhi na rasilimali nyingine kwa wazalishaji wadogo

Taasisi ya Utafiti na Utetezi wa Haki za Ardhi (LARRRI/HAKIARDHI) ni asasi ya Kiraia iliyoanzishwa mwaka 1994 na mwaka 2019 ikasajiliwa kwa usajili namba 00NGO/R2/00012 chini ya Sheria ya Asasi za Kiraia ya mwaka 2002 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2019. 

Lengo la kuanzishwa kwa HAKIARDHI ni kufanya utafiti na utetezi wa haki za ardhi kwa wazalishaji wadogo nchini ili kukuza uelewa wao katika utekelezaji wa Sera na Sheria za ardhi ili kuimarisha mifumo ya usimamizi, upatikanaji, mipango ya matumizi na utatuzi wa migogoro ya ardhi.

Salamu za rambirambi kutokana na kifo cha aliyekuwa rais wa awamu ya tano wa jamhuri ya muungano wa tanzania

Bodi ya Wakurugenzi, Wanachama, Menejimenti na Wafanyakazi wa Taasisi ya Utafiti na Utetezi wa Haki za Ardhi (HAKIARDHI) tumepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya majonzi ya kifo cha aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kilichotokea tarehe 17 Machi 2021.

HakiArdhi statement of Statement of Receipts and Expenditure

The Land Rights Research and Resources Institute (LARRRI/HAKIARDHI) is a non-governmental not for profit organization that was established in 1994 in recognition of the need to facilitate the realization of a socially just and equitable national land tenure system that promotes and advances the rights to the land of majority rural-based small producers such as peasants, pastoralists,  artisan miners and other related groups.

Uchambuzi wa athari za mabadiliko ya tabianchi na haki za ardhi Kwa wazalishaji wadogo

Mabadiliko ya Tabianchi ni mabadiliko ya hali ya hewa ya muda mrefu katika eneo fulani (Mkoa, Nchi au Bara) tofauti na iliyozoeleka. Mabadiliko hayo huleta athari katika nyanja za kiuchumi, kimazingira na kijamii. Mabadiliko ya Tabianchi ni tatizo linaliokabili dunia katika karne ya ishirini na moja na kutokana na athari zake katika nyanja mbalimbali zinazogusa maisha ya binadamu wa kawaida kila siku ikiwa ni pamoja na kilimo na ufugaji.

Wewe ni mwanamke siwezi kukupa ardhi

Simulizi ya mapambano ya haki za ardhi kwa wanawake kama ilivyosimuliwa na Frola Mgendwa wa Keiji cha Lugalo Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa

Nakumbuka ilikuwa mwaka 1994 nilikwenda kwa baba kuomba shamba, baba akasema hivii, shamba hanipi kwa sababu mimi ni mwanamke nitapata baadaye.

Wanawake kilolo wathubutu

Agnesi Kiwele wa Kijiji cha Ng'ang'ange, Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa anasimulia alivyopigania mpaka wa shamba lao akisema,

Siku moja mwaka 2018 nilienda shambani kwetu, shamba alilotuachia marehemu baba yetu. Nilipofika shambani nilikuta baba mdogo ameweka mpaka tofauti na ilivyokuwa awali.