Skip to main content
x
Heri ya siku ya Muungano

Heri ya siku ya Muungano, 26 Aprilli 2021.

Miaka 57 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzinbar.

"Muungano wetu ni msingi imara wa mapinduzi ya kiuchumi, tudumishe mshikamano wetu."

Taarifa kwa umma: yahusu mradi wa kukuza usalama wa umiliki wa ardhi na rasilimali nyingine kwa wazalishaji wadogo

Taasisi ya Utafiti na Utetezi wa Haki za Ardhi (LARRRI/HAKIARDHI) ni asasi ya Kiraia iliyoanzishwa mwaka 1994 na mwaka 2019 ikasajiliwa kwa usajili namba 00NGO/R2/00012 chini ya Sheria ya Asasi za Kiraia ya mwaka 2002 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2019. 

Lengo la kuanzishwa kwa HAKIARDHI ni kufanya utafiti na utetezi wa haki za ardhi kwa wazalishaji wadogo nchini ili kukuza uelewa wao katika utekelezaji wa Sera na Sheria za ardhi ili kuimarisha mifumo ya usimamizi, upatikanaji, mipango ya matumizi na utatuzi wa migogoro ya ardhi.

Salamu za rambirambi kutokana na kifo cha aliyekuwa rais wa awamu ya tano wa jamhuri ya muungano wa tanzania

Bodi ya Wakurugenzi, Wanachama, Menejimenti na Wafanyakazi wa Taasisi ya Utafiti na Utetezi wa Haki za Ardhi (HAKIARDHI) tumepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya majonzi ya kifo cha aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kilichotokea tarehe 17 Machi 2021.

HakiArdhi statement of Statement of Receipts and Expenditure

The Land Rights Research and Resources Institute (LARRRI/HAKIARDHI) is a non-governmental not for profit organization that was established in 1994 in recognition of the need to facilitate the realization of a socially just and equitable national land tenure system that promotes and advances the rights to the land of majority rural-based small producers such as peasants, pastoralists,  artisan miners and other related groups.

Uchambuzi wa athari za mabadiliko ya tabianchi na haki za ardhi Kwa wazalishaji wadogo

Mabadiliko ya Tabianchi ni mabadiliko ya hali ya hewa ya muda mrefu katika eneo fulani (Mkoa, Nchi au Bara) tofauti na iliyozoeleka. Mabadiliko hayo huleta athari katika nyanja za kiuchumi, kimazingira na kijamii. Mabadiliko ya Tabianchi ni tatizo linaliokabili dunia katika karne ya ishirini na moja na kutokana na athari zake katika nyanja mbalimbali zinazogusa maisha ya binadamu wa kawaida kila siku ikiwa ni pamoja na kilimo na ufugaji.

Wewe ni mwanamke siwezi kukupa ardhi

Simulizi ya mapambano ya haki za ardhi kwa wanawake kama ilivyosimuliwa na Frola Mgendwa wa Keiji cha Lugalo Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa

Nakumbuka ilikuwa mwaka 1994 nilikwenda kwa baba kuomba shamba, baba akasema hivii, shamba hanipi kwa sababu mimi ni mwanamke nitapata baadaye.

Wanawake kilolo wathubutu

Agnesi Kiwele wa Kijiji cha Ng'ang'ange, Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa anasimulia alivyopigania mpaka wa shamba lao akisema,

Siku moja mwaka 2018 nilienda shambani kwetu, shamba alilotuachia marehemu baba yetu. Nilipofika shambani nilikuta baba mdogo ameweka mpaka tofauti na ilivyokuwa awali.

Maadhimisho ya siku ya wanawake na ukombozi wa wazalishaji wadogo.

Historia ya siku ya Wanawake duniani inaonesha kuwa tarehe 8 Machi ilichaguliwa kusherehekea siku ambayo wanawake katika Urusi ya Usoviet walianza kufanya maandamano ya haki ya kupiga kura ambayo walipewa mnamo 1917. Kwa hiyo ni sahihi kusema kuwa chimbuko la siku ya wanawake iliadhimishwa tu na wanaharakati wa kijamaa na nchi za kikomunisti. Ilipofika miaka ya 1960 hususani mwaka 1967 vuguvugu kubwa la wanawake (Feminist movement) walianza kuitumia siku hii kuadhimisha siku ya wanawake.

Taasisi ya HAKIARDHI imefanya uchambuzi wa bajeti ya Wizara ya ardhi

Taasisi ya HAKIARDHI imefanya uchambuzi wa bajeti ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ya mwaka 2020/21 ili kubaini ni kwa kiasi gani bajeti hiyo inakidhi mahitaji ya wazalishaji wadogo hususani wanawake katika upatikanaji wa ardhi, matumizi, umiliki na utatuzi wa migogoro ya ardhi.

 

Mradi wa Ardhi Yetu

Taasisi ya Utafiti na Utetezi wa Haki za Ardhi (LARRRI/HAKIARDHI)  ni Taasisi ya Kiraia iliyoanzishwa mwaka 1994 kwa lengo la kufanya Utafiti na Utetezi wa haki za ardhi kwa Wazalishaji Wadogo wadogo nchini ili kukuza uelewa wao katika Sera na Sheria za ardhi na kuimarisha mifumo ya usimamizi, matumizi na utatuzi wa migogoro ya ardhi. HAKIARDHI ilisajiliwa chini ya Sheria ya Makampuni Sura ya 212  mwaka 1994 na kisha mwaka 2019 usajili ulihamishwa chini ya Sheria ya Mashirika yasiyo ya Kiserikali kwa usajili namba 00NGO/R2/00012. 

Subscribe to