Skip to main content
x

Uchambuzi wa Marekebisho ya Sera ya Taifa ya Ardhi ya mwaka 2016

Mtandao wa Mashirika yanayojihusisha na Utetezi wa Rasilimali Ardhi (TALA) pamoja na wadau wengine walikutana Jijini Dar es Salaam kufanya uchambuzi wa Rasimu ya Mapitio ya Sera ya Taifa ya Ardhi 2016. Katika kuipitia na kufanya uchambuzi wadau walibaini masuala kadha wa kadha ambayo Sera imeyajadili kwa kina na hayahitaji marekebisho, masuala ambayo Rasimu imeyajadili kwa ufinyu na yanahitaji kuboreshwa na masuala ambayo hayajaguswa kabisa na Rasimu ambayo yanahitaji kuwa sehemu ya rasimu ili kulinda haki na maslahi ya wazalishaji wadogo wadogo katika kupata, kutumia, kumiliki na utatuzi wa migogoro ya ardhi. Aidha uchambuzi unatoa tafsiri ya athari, kama vipengele hivyo vya kisera vitapitishwa kama vilivyo, pamoja na mapendekezo ya nini kifanyike.